Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana na Wenye Ulemavu inatekeleza programu ya kukuza Ujuzi na stadi za kazi stahiki ili kumuduushindani katika soko la ajira.
Miongoni mwa mafunzo yatayotolewa ni Ubunifu wa Mitindo na Ushonaji Nguo, Ufundi Bomba, Uashi, Useremala, Uchomeleaji na Uungaji vyuma, Upakaji rangi na maandishi ya alama, Utengenezaji wa vipuri vya mitambo, Ufundi Magari na Mitambo, Umeme wa majumbani na viwandani, TEHAMA, Umeme wa Magari, Huduma za Hoteli na Utalii, Madini, Kilimo na Uchomeleaji na uungaji vyuma.