Karibu

Kuhusu Vyuo na Vyuo Vikuu

Vyuo na Vyuo Vikuu ni kitengo kimojawapo kilichopo kwenye Idara ya Uhusiano wa Kimataifa , Vyuo na Vyuo Vikuu ambayo ni miongoni mwa Idara nne (4) zinazounda Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM)

Kitengo hichi kinasimamia na kuratibu shughuli zote za wanafunzi wa vyuo na vikuu, kuandaa na kutoa mafunzo ya itikadi, semina, makongamano, matamasha na warsha mbalimbali.

Majukumu

1.

Kuwajenga wanafunzi katika maadili ya uzalendo, umoja na utaifa. Pia kuthubutu kutenda katika mazingira ya maendeleo ya Sayansi na Teknolojia.

2.

Kuunga mkono na kushiriki kikamilifu katika ukuzaji na uendelezaji wa vipaji na taaluma za wasomi kwa lengo la kuimarisha moyo wa uvumbuzi miongoni mwa jamii ya vijana wasomi wa Taifa.

3.

Kukuza uhusiano na ushirikiano baina ya Vyuo na Vyuo Vikuu na Taasisi za hiari zinazojishughulisha na masuala ya elimu, sayansi na utamaduni ndani na nje ya Tanzania.

4.

Kuwa chemchem ya fikra na mawazo ya kimaendeleo kwa Taifa.

5.

Kufanya tafiti za changamoto zinazolikabili Taifa.

Mawasiliano

Opening Hours

24/7