Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipata maelezo kuhusu uandaaji wa Nyama mara baada ya kuzindua kiwanda cha Nyama cha Eliya Food Overseas LTD kiliopo Eurendeke Longido Mkoani Arusha leo tarehe 18 Oktoba 2021. Mhe. Rais Samia yupo Mkoani Arusha akiendelea na ziara yake ya kikazi kutembelea, kukagua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo ya Wananchi Mkoani Arusha.