Machi 26, 2022 Tawi la UVCCM chuo cha Usafirishaji (NIT) liliandaa darasa la Mapinduzi ya fikra na Ujasiriamali lenye lengo la kumbadili kijana wa chuo kifikra na kumpa elimu ya ujasiriamali ili kuleta ukombozi wa hali (kiuchumi) na kiutendaji, kuwa chombo na kielelezo cha kuleta maendeleo katika familia, chama, jamii na Taifa kwa ujumla wake.